Customer Feedback Centre

Ministry of Health

WAZIRI UMMY ATETA NA BALOZI IRELAND KUHUSU UBORESHAJI SEKTA TA AFYA KUPITIA MFUKO WA AFYA WA PAMOJA

Posted on: June 4th, 2023

Na. WAF - Dar es Salaam

Waziri Ummy na Balozi wa Ireland nchini Tanzania Mhe. Mary O’Neillleo wamekutana leo June 4, 2023 na kufanya mazungumzo katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam

Katika kikao hicho Waziri Ummy na Balozi na Mhe. Mary O’Neill wamejadili masuala mbalimbali ya Ushirikiano katika kuendeleza Sekta ya Afya nchini hususani katika mfuko wa Afya wa pamoja (Health Basket Fund) na changamoto zinazoikabili Sekta ya Afya.

Aidha, Waziri Ummy ameweza kubainisha changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta ya Afya nchini na namna gani wameendelea kushirikiana na Ubalozi wa Ireland katika kuhakikisha changamoto hizo zinatatuliwa ikiwemo kuja na programu zinazoweza kuboresha Sekta hiyo katika utoaji wa huduma za afya.

Kwa upande wake Balozi wa Ireland Nchini Mhe. Mary O’Neill amesema nchi hiyo itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta afya ambapo wameanza utekelezaji katika mpango kazi wao wa mwaka 2022/2026.