Maoni Ya Wateja

Wizara Ya Afya

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA KSI CHARITABLE EYE CENTRE KUIMARISHA HUDUMA ZA MACHO NCHINI

Posted on: July 1st, 2024



Serikali kupitia Wizara ya Afya imeahidi kushirikiana na Taasisi ya Khoja Shia Ithna ili kuimarisha huduma za macho nchini ikiwemo utoaji wa huduma ya upasuaji mdogo, vipimo pamoja na kutoa miwani katika makundi mbalimbali ya wananchi wenye uhitaji wa huduma hizo.


Hayo yamesemwa Juni 30, 2024 na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa hafla ya uchangiaji fedha kwa ajili ya kununua vifaa vya kisasa na kuboresha miundombinu katika Taasisi ya Khoja Shia Ithna Asheri Charitable Eye Centre iliyopo Manispaa ya Temeke jijini Dar es salaam.


Waziri Ummy ameipongeza Taasisi hiyo kwa kuendelea kuwahudumia Watanzania kwa kufikisha huduma hizo karibu na sehemu wanazoishi huku akiahidi kuendelea kuwapa ushirikiano wa karibu ili waweze kutimiza malengo yao na waendelee kushirikiana na Serikali katika kuimarisha utoaji wa huduma za Afya nchini.