Customer Feedback Centre

Ministry of Health

SERIKALI NA USAID KUSHIRIKIANA KUTIMIZA VIPAUMBELE VYA SEKTA YA AFYA

Posted on: February 29th, 2024



Na WAF – DODOMA

Serikali kupitia Wizara ya afya imeadhimia kuendelea kushirikiana na shirika la Kimataifa la Maendeleo la Marekani USAID kwa mwaka 2024/25 kusaidiana kutimiza vipaumbele vya sekta afya na kuboresha hali ya utoaji wa huduma za afya Nchini.

Hayo yamebainishwa Februari 29, 2024 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. John Jingu wakati wa kikao cha mapitio ya portfolia kati ya Serikali ya Tanzania na Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID)ambapo amesema katika kuboresha huduma za afya na kuondokana na changamoto ambazo ni kikwazo kwa wananchi ni muhimu kutambua mchango wa wadau wa afya na maendeleo.

Dkt. Jingu amesema USAID imekuwa ikishirikiana na Serikali ya Tanzania katika nyanja mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Uzazi wa Mpango, Afya ya Kina Mama na Watoto, Usalama wa Afya wa Kimataifa, usimamizi wa ugavi, na mifumo ya taarifa za afya.

“Kwa miaka mingi, Serikali ya Tanzania na USAID wamekuwa wakishirikiana katika miradi mbalimbali ya afya, ikiwa ni pamoja na mipango ya kupambana na VVU na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria, Uzazi wa Mpango, Afya ya Kina Mama na Watoto, kuimarisha mfumo wa afya, na Usalama wa Afya wa Kimataifa. Kwa msaada wa USAID, Serikali ya Tanzania imefanikiwa kupanua huduma kamili za VVU katika mikoa 14”. Amesema Dkt. Jingu

Aidha amebainisha ni muhimu kwa USAID kuelewa vipaumbele vya afya vilivyowekwa na Serikali ya Tanzania ili kuongeza athari yetu pamoja na kukuza mabadiliko muhimu katika kushughulikia pengo la Rasilimali Watu kwa Afya, kutekeleza bima ya afya ya kimataifa, kuboresha ubora wa huduma za afya, kusaidia Watoa Huduma za Afya za Kijamii, kupambana na Maradhi Yasiyoambukiza, na kuimarisha ushirikiano wa umma na binafsi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Misheni ya USAID Bw. Craig Hart amesema Shirika la Maendeleo la USAID litaendelea na ushirikiano katika kuleta matokeo chanya na yenye athari katika afya na ustawi wa Watanzania.

Vipaumbele hivyo vitakamilishwa na jitihada za kushughulikia tofauti za afya, kuchochea usawa wa kijinsia, kuingiza masuala ya afya katika sera zote, na kuboresha upatikanaji wa huduma za afya bora kwa wote bila kuweka m