Maoni Ya Wateja

Wizara Ya Afya

WAJAWAZITO WAHAMASISHWA KUWAI KLINIKI MAPEMA

Posted on: November 10th, 2022

Na. WAF - Dodoma 


SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imetoa wito kwa Wajawazito kuhudhuria kliniki mapema kwa lengo la kupata muda wa kutosha kwa Wataalamu kufanya uchunguzi na ufuatiliaji ili kuondoa dharura za kufanyiwa upasuaji wakati wa kujifungua. 


Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel katika kikao cha tisa cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Mhe. Dkt. Christina Mnzava.


Amesema, Serikali inaendelea kutimiza jukumu lake la kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto, hivyo kutoa wito kwa Wajawazito kujenga tabia ya kuwahi mahudhurio ya kliniki na kufanyiwa uchunguzi ili kujua hali zao mapema.


Aidha, Dkt. Mollel amesema, Serikali itaendelea kutoa elimu kwa wananchi, hususan wajawazito kupata lishe bora ili kujenga mtoto mwenye afya njema na kumlinda dhidi ya magonjwa. 


Akijibu swali la Dkt. Alice Kaijage kuhusu upungufu wa Wataalamu wa mazoezi tiba na utengamao Dkt. Mollel amesema, Serikali imeajiri jumla ya Wataalamu 84 wa mazoezi tiba na huduma utengamao katika ajira za mwezi Julai 2022 na hivyo kufanya idadi ya wataalamu wa mazoezi tiba na huduma utengamao kuongezeka kutoka 653 hadi 737.


Hata hivyo Dkt.  Mollel amesema Kwa sasa kuna jumla ya vyuo vikuu vinne (Muhimbili, KCMC, Bugando na Zanzibar) vinavyotoa taaluma hivyo kupunguza changamoto ya uwepo wa Wataalamu katika soko la ajira.


Mwisho.