Maoni Ya Wateja

Wizara Ya Afya

WAZIRI UMMY AKUTANA NA MWAKILISHI MKAZI KUTOKA UN-WOMEN

Posted on: June 16th, 2022

Kutoka Dodoma, Juni 17, 2022.


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu leo Juni 17,2022 amekutana na kufanya mazungumzo na mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa upande wa wanawake (UN - WOMEN) katika ofisi za Wizara Jijini Dodoma. 


Katika mazungumzo yao kwa pamoja wamekubaliana kushirikiana katika masuala ya afya, hususan katika kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto na usawa wa kijinsia katika Sekta ya Afya. 


Waziri ummy amempongeza Mwakilishi huyo kwa kazi nzuri anazoendelea kufanya na ameahidi kuendelea kushirikiana nae ili kufikia malengo ya kuboresha huduma za afya hasa zinazowahusu wanawake katika Sekta ya Afya. 


#AfyaKwanza 

#JaliAfyaYako